Forex trading ni nini? (introduction)

FOREX NI BIASHARA YA UBADILISHAJI WA FEDHA ZA KIGENI AMBAYO IMEONEKANA KUWA NA MZUNGUKO MKUBWA ZAIDI KULIKO BIASHARA YOYOTE DUNIANINI KWANI INAZUNGUSHA ZAIDI YA DOLLA ZA KIMAREKANI TRILLION 5 KWA SIKU.
HII NI BIASHARA AMBAYO IMECHANGIWA SANA NA MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA AMBAPO SASA MTU YEYOTE UNAWEZA UKAFANYA BIASHARA HII AMBAPO KUNA MTANDAO WA INTANETI KAMA KOMPYUTA NA SIMU JANJA(smartphone)

Introductory Lesson (Somo la Kiutangulizi) kuhusu Forex kwa malengo matatu hivi:

1. Kuwapa hamasa wale ambao bado hawafanya uamuzi wa kujiunga na Forex,
2. Kuwapa mwanga wale waliojiunga lkn bado hawaielewi biashara hii, na
3. Kurekebisha mawazo ya wale wenye uelewa usio sahihi.

Tuanze,...

Naamini tayari unaelewa kwamba:
1. Forex ni kifupisho cha FOReign EXchange kwa maana ya biashara ya kununua na kuuza fedha za kigeni. Kama unavyoijua kazi ya Bureau de Change, ndiyo iyo hiyo tunaifanya kwenye Forex sema hii ni ya mtandaoni.
2. Forex ni biashara halali na inafanyika ulimwenguni mwote na taasisi kubwa kubwa za kifedha na mabenki na central banks.
3. Biashara hii ni ya mtandaoni na wauzaji na wanunuzi hukutana huko ~soko lake ni la mtandaoni na ni la dunia nzima. Inakadiriwa kuwa, biashara hii imevutia wawekezaji ambao kwa pamoja (wakubwa na wadogo) wanaTRADE zaidi ya US Dollars Trilioni 5.3 kila siku!
4. Hii biashara kwa kuwa ni ya mtandaoni, ukitaka kuifanya ni lazima uwe na fedha mtandaoni. Unafungua account mtandaoni kama unavyofungua bank, unaweka fedha zako. Unazifanyia biashara na siku ukitaka kuzitoa, unazitoa mtandaoni zinakuwa cash za kutumia.
5. Biashara hii, kwa kuwa ni ya mtandaoni, unaweza kuifanyia popote! Nyumbani, chumbani, njiani, sokoni..popote! Unahitaji tu vitu vitatu:
a)Computer/Laptop ambayo itakusaidia kuliangalia soko na kujua muelekeo (Market Analysis)
b) Internet connection. Kwa sababu ni biashara ya mtandaoni, unahitaji kujiung na mtandao.
c) Programu maalum yenye uwezo wa kusoma soko. Hii inaitwa Trading Platform. Hii ni software ambayo, unai~download na kui~install kwenye Computer yako. Hizi ziko nyingi sasa lakn moja maarufu ambayo inatumika sana duniani inaitwa Meter Trader 4 (MT4).

Note 1: Ni lazima uwe na Computer/Laptop na ui~install MT4 kama unafanya Market Analysis mwenyewe lkn, kama kuna mtu mwingine anaweza kufanya kwa niaba yako na akakupa kile tunaita Trading Signal, sio lazima uwe nayo. Unaweza tu ukawa na simu yako au gadget yoyote ile inayoweza kuunganishwa na mtandao. Uzuri, hata MT4 nazo, zumetengenezwa mpaka za simu hivyo, unaweza kui~install ktk simu na ukaendelea kuTRADE.

Note 2: Baada ya kutimiza hayo, kabla hujaanza KUNUNUA NA KUUZA fedha za kigeni mtandaoni, Ku~Trade Fore x, unamuhitaji mtukati anayeitwa Broker. Kwanini? Nitafafanua zaidi pale chini lakini, kwa hapa niseme tu, ndiye anayesimama kama bank ya mtandaoni kwako. Utafungua account kwake kama unavyofungua account NMB, NBC, Equity, Exim, n.k. Utampatia taarifa zako zote rasmi, Vitambulisho vyote muhimu, Uraia, Anuani ya unapoishi,...kila kitu. Ndipo atakuruhusu kufungua account ya mtandaoni. Niwaonye wanaopenda kudanganya, hapa usijaribu, utafeli. Hapa wanahitaji taarifa zako halisi na sahihi. Hii ni kwa sababu, hii ni biashara halali kabisa, na ni ya dunia nzima na, inakupatia kipato halali. Sasa, siku umepata faida unataka kuzitoa pesa zako, watakuambia hatukupi maana si wewe, endapo utawasilisha utambulisho mwingine tofauti na ule uliojazaga. Baada ya kuifungua account kwa Broker, unaweka hela zako humo, labda USD, GBP, JPY..utakavyo mwenyewe. Baada ya hapo, sasa upo tayari kuanza biashara.

Huo ulikuwa Utanguli wa Hatua Muhimu kabla hatujaingia Sokoni. Sasa twende Sokoni. Twende kwa Hatua pia:

1. Forex inafanyika kwa kulinganisha thamani za Sarafu Mbili kwa pamoja (Currency Pairs).
Kule sokoni unapoingia, ili uweze kununu na kuuza, utakuta bidhaa (currency) zimewekwa kwenye mafungu mafungu ya mbili mbili (pairs). Mfano:
i)Euro na US Dollar pamoja,
ii) Paund (GBP) na USD pamoja,
iii) USD na Yen (JPY) pamoja,..nk. nk. nk
Zinavyopangwa, utazikuta hivi:
EUR/USD
USD/JPY
GBP/USD
USD/CAD
.
.
Chukua EUR/USD kwamfano;
Hiyo ya mwanzo (EUR) Inaitwa BASE currency, na hiyo ya pili, USD, unaitwa COUNTER Currency. Sasa, bei unazoziona kwenye grafu zikipanda na kushuka ni bei za Base Currency kwa kulinganishwa na Counter Currency. Chukulia hii;

EUR/USD = 1.25358

Maana yake, Euro 1 = 1.25358 USD. Kama unataka kununua EURO 1, utalipa
1.25358 USD.

Bei za Euro sokoni, kwa kulinganishwa na USD, zinaweza kubadilika ndani ya sekunde! Sasa, faida zinapatikana kwa wewe KUNUNUA Currency moja, wakati bei iko chini na KUIUZA wakati bei inapopanda. As Simple as that. Sasa, ili kujua kwamba baada ya muda itapanda ili UNUNUE sasa hivi na uuze itakapopanda, au, kujua kwamba itashuka zaidi ya hapo ilipo ili, UUZE sasa hivi na UNUNUE itakapofika bei ya chini zaidi,...mchakato huo unaitwa MARKET ANALYSIS.

2. Forex Trading, hufanyika kwa "Kubonyeza tu" kitufye cha kuBUY au cha kuSELL. Basi. Hilo tu. Unakuwa umefanya TRADE. Lakini sasa, ili uweze kujua, unabonyeza kipi, muda gani, uTRADE kiasi gani ili upate faida gani, inabidi uwe unajua kufanya MARKET ANALYSIS mwenyewe au uwe na MTAALAMU unayemuamini akufanyie na akupe taarifa hiyo. Sasa, hiyo taarifa ndiyo inaitwa "Fx Signals" au "Trade Signals"..nk.

3. Faida au hasara kwenye Forex Trade zinapimwa kwa PIPS.

PIP ni kitu Gani? Kitefu chake ni "Percentage In Point". Pip ni tofauti ya POINT MOJA katika bei ya Pair ya Currency tokea ulipoweka ORDER yako. Its a 1point Price Movement ama kwenda juu au kuja chini.

Hii tofauti ya bei (Pip) inapimwa katika viwango vya Desimali. Currency Pairs nyingi (sio zote tafadhali) zinatumia SEHEMU NNE ZA DESIMALI. Utakuta kwenye Platform wanaandika SEHEMU TANO lakini ni ili kukusaidia wewe mfanyabiasha, ila zinazohesabika ni NNE.

Utaelewa vizuri kwenye mfano. Chukulia hiyo ya pale juu:

EUR/USD = 1.25358

Tunaangalia "Price Movement" katika sehemu ya 4 ya desimali. Ile ya tano inakupa tu sehemu ya Pip.

Chukulia hapo bei ibadilike ama kwenda juu au chini kama ifuatavyo:


EUR/USD = 1.25458
:arrow_up:
EUR/USD = 1.25358
:arrow_down:
EUR/USD = 1.25258

:arrow_forward: Kutokea 1.25358 kwenda 1.25458 maana yake bei imepanda kwa 10pips.

:arrow_forward: Kutokea 1.25358 mpaka 1.25258 bei imeshuka kwa 10pips.

Swali, je kutoka 1.25258 mpaka 1.25200?

Jibu, imeshuka kwa 5.8pips. Sawa mpaka hapo?

Kwa hiyo, FAIDA na HASARA katika Forex zinapimwa kwa PIPS. Ukiwakuta watu wanaambiana, mimi leo nimepata, 30 USD, 50 Yen, 70 Paunds...unajua tu hawa sio professionals. Kule watu wanajisifia Pips sio Dola au Paundi au Yen. Utakuta mtaalam anasema, Mimi ninapata Average/Wastani wa 500Pips, au 700Pips au 1100Pips kwa wiki au kwa mwezi, nk. Sio Dola! Na mtaalamu anayependwa na wateja,..Anayeaminiwa kwamba anao uwezo wa Market Analysis mzuri ni yule anayejikusanyia PIPS nyingi mwisho wa siku.

Swali: Je, naweza kupata PIPS kidogo na nikawa na faida KUBWA kuliko aliyepata PIPS nyingi kunizidi?

Jibu: Ndio. Inawezekana! Lakini, wooote, tutakujua kwamba huna PROFFESSIONALISM bali umeRISK sana na ungeweza ukapoteza hela nyingi sana pia! Sema tu bahati yako leo. Hakuna mtu mwenye hela zake atakayekuamini tukikujua hivyo. Nitaeleza zaidi hili sehemu inayofuata.

5. Nini Thamani ya PIP moja? Ili nijibu hili swali, kuna maelezo lazima nikupe. Ila kwa kifupi, thamani ya PIP moja inaweza kuwa ni 10 USD, au 1 USD, au 0.1 USD. Angalia:

Kumbuka, hii ni biashara kubwa sana. Kule kwenye soko la dunia, CURRENCY zinauzwa kwa jumla. Huwezi kwenda kununua eti Dola 1, au Paundi 5 au Euro 8. No. Unanunua kwenye mafungu! Kule kuna mafungu matatu tu maalum yanayouzwa:

a) 100,000 USD, au
b) 10,000 USD, au
c) 1,000 USD

Kwani hata Buteau de Change si wanauza kwa mafungu? Utakuta;

1 - 50 USD bei yake
51- 100USD bei yake
101- 1000USD bei yake
N.k. nk, nk..ndo ivo ivo kule.

Sasa,..

Wale waliosoma Science Sekondary mnikumbushe hii: S.I Unit maana yake nini tena? International Standard Unit? Nimesahau. Ila maana yake ni hii. Kipimo maalum kilichokubalika dunia nzima kupimia kitu mfano;
Urefu, S.I.Unit ni Meter
Ujazo, S.I.Unit ni Litre
Uzito, S.I.Unit ni Gram
N.k, n.k,...

Sasa kwenye Forex, kipimo kilichokubalika kupimia kiwango cha MAFUNGU ya kuuza na kununua Currency kinaitwa "Lot" Tumezoea kuita, "Standard Lot".
:arrow_right: Lot moja ukiigawa kwa KUMI utapata 1 Mini~Lot.
:arrow_right: Mini~Lot moja ukiigawa kwa KUMI (au Standard Lot moja ukiigawa kwa MIA) unapata 1 Micro~Lot.

Angalia sasa;

1 Std Lot = 100,000 USD,
1 Mini~Lot = 10,000 USD
1 Micro~Lot = 1,000 USD

Nenda kinyumenyume, utaona kwamba:

1lot = 10 mini~lots = 100 micro~lots

Au kwa namna nyingine;

1Micro~lot = 0.1 Mini~lot = 0.01lot.

Sasa, unapokwenda KUPLACE ORDER ya kuBUY au kuSELL kuna sehemu utaulizwa ujaze SIZE ya ORDER yako. Utajaza 1Lot kwa maana ya unanunua au kuuza 100,000USD au utajaza 0.1lot kwa maana ya unauza au kununua 10,000USD au utajaza 0.01lots kwa maana ya unauza au kununua 1,000 USD.

Sasa twende kwenye thamani ya PIP.

Endapo ULIUZA au KUNUNUA "1 Standard Lot", kila PIP moja unayoipata sokoni kama faida, ni sawasawa na 10 USD. Maana yake, kwa 100,000 USD ulizoTRADE, umepata faida ya 1PIP au 10 USD.
Kama uliTRADE 1minilot, 1PIP ni sawa na 1 USD na kama uliTRADE 1 microlot, PIP moja ni sawa na 0.1 USD.

Umenielewa mpaka hapo? Ngoja nikusisitize yafuatayo kama NB.

Note1: Si kila Currency Pair PIP yake inapimwa kwa 4decimal places. Kuna baadhi sio, mfano Currency Pairs ambazo zina Japaneese Yen ndani yake kama EUR/JPY au USD/JPY na zingine, PIP yake moja inahesabiwa katika sehemu MBILI za Desimali. Ukishakuwa sokoni utazizoea tu usiogope. Utazijua zote.

Note 2: Sio kila 1PIP ni sawa na 10USD kwa 1lot. Kuna tofauti zake pia. Baadhi ya currency pairs, 1lot zao, 1PIP utakuta ni 8USD, 11USD au hata 7USD. Inategemea. Ile ya 1Pip = 10 USD ni Standard. Utazielewa pia ukishaingia sokoni. Ila mpaka hapa, unaweza kuelewa kwamba, aliyepata 25pips za 1lot za:
i) EUR/USD,
ii) EUR/JPY, na
iii) GBP/USD
wanatofautiana kwenye hela kwa sababu thamani ua 1PIP kwao zinatofautiana. Ila tofauti zao si kubwa saaana. Zoote, zinakaribi pale pale kwenye Kwa 1std lot, 1Pip = 10 USD.

6. Hivi Kweli, kuna Retail Trader ataweza kununua 1lot, au 1minilot, au hata 1microlot (kiasi cha chini kabisa cha order moja ambacho ni 1000usd = 2.4mil Tzs) na akasavaivu kwenye hii biashara kweli. Huko si ni kubaguana? Wataifanya wenye nacho tu, si ndiyo?

Hapo sasa, ashukuriwe Mungu kuna Mtukati anaitwa Broker. Ndiye anayetuwezesha mimi na wewe tushiriki Forex. Vingenevyo, ingebaki kuwa ni biashara ya Mabenki, Serikali, Taasisi kubwa kubwa za Kifedha ma Matycoon wakubwa.

Kazi kubwa ya Broker ni kukukopesha hela zake ili uzifanyie biashara ya Forex. Atakuambia kwamfano; ukifungua account ya mtandaoni kwangu, uka~deposite hela, kwa kila Dola 1 utakayo~deposite, nitakukopesha Dola 100 au, 200, au 500 au wengine mpaka 1000! Hicho kitendo kinaitwa "Leverage". Wanaandika hivi:

Leverage:
1:50 (kwa kila dola 1 uyakayoweka kwangu, nakukopeaha 50), au
1:100 (weka 1, kopa 100), au
1:500 (weka 1 kopa 500) n.k, n.k

Kwamfano sasa, ukiweka USD 100 kwenye account yenye Leverage ya 1:500 maana yake ni nini?

Kwa kila dola 1 uliyo~deposite anakukopesha dola 500. Kwa hiyo, jumla utakuwa na dola 100 x 500 = 50,000. Hiyo inaitwa "Purchasing Power". Hapo maana yake ni kwamba unauwezo sasa wa kununua au kuuza USD 50,000 ambayo ni sawa na 0.5 lot size, tofauti na awali ambapo ungetegemea 100$, usingeweza kuuza au kununua chochote (hata order ndooogo kabisa ambayo ni Micro~Lot = 1000usd).

Brokers wanakuchaji wewe comission wakati wowote unapoTRADE, ndipo kipato chao kilipo. Siku nyingine nitawazungumzia kwa undani kidogo hawa maBroker. Kwa leo niishie tu hapo.
Je, hii biashara ina muhimu wowote kwako? Jibu linategemea wewe unahitaji nini
1. Kama unataka soko ambalo halilali.
2. Kama unataka fursa ya kufanya biashara mda wowote katika siku.
3. Kama unataka kutengeneza kiasi kikubwa cha pesa.
Basi nadhani FOREX ni mahala sahihi kwa hayo yote
NB: Kama utaweza tengeneza kiasi kikubwa cha pesa ndani ya mda mfupi, pia unaweza kupoteza kiwango cha fedha ndani ya mda mfupi huohuo
Watu gani wanaokuwepo/wanaoshiriki katika hii biashara?
1. Benki kuu (Central banks)
2. Serikali (Government)
3. Umoja wa wawekezaji(investment coorperation)
4. Wafanyabiashara wa duniani kote(businessies worldwide)
5 Wafanyabiashara wadogo(Retail trader)
Maeneo vitovu katika hii biashara duniani ni:
1. NEW YORK (United States Dollar USD)
2. LONDON (Euro EUR and Pound GBP)
3. FRANKFURT (France franc CHF)
4. TOKYO (Japanese YEN JPY)
5. SYDNEY(Austarlian dollar AUD)
Soko la FOREX hufunguliwa jumapili saa 6 usiku na kufungwa Ijumaa saa 5:59 usiku hivo ndani ya huu mda una uwezo wa kufanya biashara
FAIDA ZA FOREX
1. Una uwezo wa kufanaya biashara sehemu yeyote ulipo
2. Unaweza kutoa faida hela zako mda wowote ndani ya siku za wiki.
3. Sheria rahisi.
4. Inapatikana masaa 24
5. Uwiano mzuri kwa kiasi kidogo unaweza ingiza faida kubwa. (Leverage)
6. Upatikanaji wa FAIDA kubwa na kwa haraka.
 Kwa miaka kadhaa mpaka sasa, kumekuwa na list kubwa ya watu wakiingia katia hii platform ya forex na ndoto kubwa ni kupata uhurru wa kifedha na kukua kiuchumi kutokana na hadithi/myths za kutamanishwa kupitia mitandao au jamaa zao wa karibu.
Forex ni kama fani nyingine. Inahitaji kusoma, kufanya majaribia, kuifatilia kwa karibu na kw juhudi ndipo uje utengeneze hela. imenichukua zaidi ya miezi 6 mpaka kuja kuanza kutengeneza faida.
 
2. AINA YA WAFANYABIASHARA KATIKA FOREX.
Hii ni eneo muhimu sana kulijua na wewe kufanya maamuzi unataka uwe mfanyabiashara wa aina gani. Hivyo kabla hujaanza ni bora kujitathmini wewe ni mfanyabiashara wa aina gani na utumie njia zipi katika kufanya biashara yako.

Forex lesson tanzania (swahili)
1. SCALPER
Huyu ni mfanyabiashara anaekuwa katika soko kwa mda mfupi sana. Mara nyingi anaingia na kutoka katika trade na dakika kadhaa tu. Kivutia kikubwa kwa trader wa aina hii huona faida au hasara ndani ya mda mfupi tu. Msingi mkubwa wa scalper ni kuwa na uwezo wa kufikiri haraka na kuweza kumantain pressure. Kulingana na mda mfupi wa fursa scalper huamua aingie katika hio fursa au aache


2. DAY TRADER
Huyu ni trader ni yule ambae huingia katika trade siku husika na kutoka katika trade siku hio hio.Tofauti na scalper, yeye huingia katika trade na kuisubiri ndani ya dakika 30 au saa. Uzuri wa kuwa day trader ni mda wa kutosha wa kufanya zako analysis. mara nyingi huwa na mda maalum wa kuingia katika trades zake. Na mda ukifika wanasubiri fursa ijitengeneze na kuingiza trades zao, hutumia dakika 30, saa moja mpaka saa 4 timeframe kufanya analysis zao.

3. SWING TRADER
hawa ni traders wanaofanya biashara kila siku.... kwa kua kila siku kunakuwa na nafasi za mtiririko/swings katika soko. ukitokea mtririko wa kupanda wanapanda nao.. ukitokea wa kushuka wanashuka nao. Hawa wanafocus sana katika kuangalia mtiririko wenye asili ya uimara zaidi. na mara nyingi hutokea katika kufunguliwa kwa soko la london (London open) na New York open.Hawa wanafanana sana na day trader huwa wanaingia na kutoka katika soko ndani ya siku husika

4. POSITION TRADER
Hawa huingia katika trade kwa siku kadhaa au week. Hii ni aina nzuri kwa wale ambao hawana mda wa kuangalia chart kila siku.
Hawa pia tunaambiwa ni traders ambao wanachukua profit sana ukizingatia wanakua kwenye market kwa mda mrefu hivo kuchukua faida ya week au mwezi. Hivyo aina hii ni kwa wale wenye mitaji mikubwa